Real Madrid wanaamini kwamba teyar wameshashinda mbio za kuinasa saini ya Mbrazili Rodrygo, Huku Barcelona wamekuwa wakimfukuzia kinda huyo mwenye umri wa miaka 17 ambae amechukuliwa na klabu iliyomo kwenye nchi yake Santos msimu uliopita.
Lakini Madrid wanaonekana wameweka vyema ngome zao za kuweza kumnasa kinda huyu kwa dili la Pauni Milioni 40 kwajili ya kumdondosha Mbrazili huyu Bernabeu.
Kupitia Gazeti la Marca limesema kwamba mabingwa hawa wa Ulaya teyari wameshapiga pini vikwazo vyote vya Barcelona na kufanya mambo yote kuwa poa kwenye kufanya biashara hiyo na uongozi wa Santos.
Na inaelezwa kwamba mshambuliaji huyu ameweza kufanya vyema msimu uliopita na amepewa uhakika wa kuweza kujiunga na Real Madrid na kama Madrid wakifanikiwa kufanya biashara hii watakuwa wameokota Embe Dodo kwenye Mnazi na kuwaumiza kichwa wapinzani wao.
Barcelona wameweza kuweka nguvu zao nyingi kwajili ya kumpata Rodrygo ambae ameshinda magoli matano kwenye michezo kumi na moja ya Santos.
Home
Unlabelled
Unyama Unyama tuu..! Real Madrid yaipiga kikumbo Barcelona kwenye dili la Pauni Milioni 40 kwa kijana wa Santos Rodrygo.
Unyama Unyama tuu..! Real Madrid yaipiga kikumbo Barcelona kwenye dili la Pauni Milioni 40 kwa kijana wa Santos Rodrygo.
Share This
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Bwherever is a Tanzanian Radio Personality and Blogger who initiative Bbaseonpoint blog.
No comments:
Post a Comment