Joe jackson alikuwa ni baba wa watoto 11 pamoja na Janet Jackson na wengine watano aliunda kundi na lilisaidia kuwaongoza kwenye mafanikio mbali na hiyo pia aliweza kuunda tabia ya kutobaguana ambapo alikuza heshima kwa watoto wake ilikuweza kufikia mafanikio.
Jackson ndio alikuwa kati ya Jackson wakubwa waliobakia kwenye ukooo wao alizaliwa kwenye nyumba moja hivi ambayo ilikuwa imechakaa na baba yake Samuel Jackson na mama yake Lee akiwa na umri wa miaka 12 wazazi wake walitengana na Joe akaenda kuishi na baba yake kwenye mji wa Oakland alipofika miaka 18 alienda kwenye mji wa Chicago kuishi na mama yake na kufanya kazi kwenye kiwanda kimoja kwenye mji huo.
Kiuhalisia Jackson yeye binafsi alitaka kuwa mwanamasumbwi lakini maisha yalibadilika baada ya yeye kukutana na Katherie Scruse walifunga ndoa November 1949 na mwaka baadae aliweza kununua nyumba kwenye mji wa Gary akiwa na mtoto wake wa kwanza Rebbie.

Lakini mnamo kwenye miaka ya 60 Joe alianza kuwakuza watoto wake watatu ambao walikuwa wakubwa kuja kuwa wanamuziki na ndugu zake wadogo akiwemo Michael na Marlon ambao walikuwa wanaimba nyuma yake lakini pale alipomsikia Michael anaimba mabadiliko yakafanyika haraka Michael akawa anaongoza vocal huku kaka yake akiwa nyuma yake na hapo ndipo wakaanza kupata mashavu ya ndani ambapo ikiwapelelkea kubadilisha jina la kundi lao na kujiita Jackson Five Shortly badala ya Jackson Brothers..
Kutokana na kifo chake Joe alikuwa bado ni mume halali wa Katheine lakini waliishi kwa kutengana pia alikuwa na mjengo wake kwenye mji wa Las Vegas ambapo mke wake alikuwa akiishi Calabasas ambapo yupo na watoto wa Michael Jackson anawaangalia ambao ni watatu.
Joe pia alikuwa ni baba wa Joh Vonnie Jackson mwenye umri wa miaka 43, pia Cheryl Terrell ambae alimpata kwenye mahusiano ya mda mrefu akiwa anamiaka 25
Lakini akiwa na Katherine alifanikiwa kuwa na Maureen,68, Jackie,67, Tito,64, Jermaine,63, La Toya, 62, Marlon,61, Randy,56 na Janet 52 huku Michael yeye alikufa akiwa na miaka 50 Juni 25 2009.
No comments:
Post a Comment