“Mimi jamani ningekuwa naogopa macho ya watu basi nisingesonga mbele....."-ODAMA - BZONE

“Mimi jamani ningekuwa naogopa macho ya watu basi nisingesonga mbele....."-ODAMA

Share This
Nyota wa filamu Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amefunguka kuwa ‘ukauzu’ wa kufanya jambo bila kumhofia mtu ndio umemfanya afike mbali kimaisha.

 Odama alisema kuwa kuna watu wengi hasa mastaa wanaogopa macho ya watu hivyo hata kama wapo kwenye shida fulani wanajivunga tu na kujisababishia matatizo mengine kwa kushindwa kuikubali au kuipokea hali ambayo wanakutana nayo kwa kipindi hicho.



“Mimi jamani ningekuwa naogopa macho ya watu basi nisingesonga mbele kabisa lakini sikujali na hata nikianguka siangalii mtu ameniangaliaje, napambana kuinuka upya,” alisema Odama.

Mrembo huyo ni miongoni mwa warembo wachache Bongo ambao wanamiliki kampuni binafsi ya kuzalisha filamu, kampuni yake inaitwa J-Film 4 Life.

No comments:

Post a Comment

Pages