Wote kwa pamoja walisimama mikono yao ikiwa kwenye mifuko wakiwa wanazunguka kwenye eneo lao la ufundi ilionekana ni motisha ya kuwasogeza mbele.
Ikiwa kama picha ambayo iliwahukumu wote kwa pamoja tukiwa tunaongelea mda wote wanapokutana wakichukilia ni mashindano makubwa na alizani kwa vijana aliokuwa nao au aliowapanga wanaweza wakaimili ile mikiki.
Klopp alikuwa na muonekano dhaili wa kukata tamaaa na sio kama siku zote tulivomzoea au ilikuwa ni moja ya mipango yake maana ata magoli yalipokuwa yanaingia yeye alitulia tu.
Guardiola alikuwa ni bandia kabisa alikuwa ni kinyume cha Guardiola tunayemjua alikuwa tofauti sana kama sio siku zote tulivomzoea alikuwa amepakwa rangi ya kijivu na nyeusi kwenye mwili wake.
Sawa ata kwenye benchi lake la ufudni lilikuwa limebanwa midomo kwa pini yenye kutu sikujua walikuwa na nini kwa siku ya jana hasa pale city walipo wapa zawadi Liverpool ya goli la kwanza ambalo liliwafanya watengane na kuzalisha zaidi ya lile walilopata.
![]() |
| oxlrade-Chamberlain akishangilia bao lake |
Guardiola alianza kupata matumaini na kuanza kutunisha misuli kwa kuwaweka kwenye presha kubwa Liverpool alivopigwa ata lile kwanza Muhispania alikuwa anacheka tuu na bado alikuwa na nguvu za kupiga kelele za matumaini akijifanya anaendelea kuwasukuma wasogee mbele.

Kwenda kule mbele na kushambulia alijisahau kuwa huku nyuma ameacha mianya City walionekana bado wanaweza wakamudu mikiki na bado wanauwezo wa kurudisha sasa pale Liverpool walipovunja tuu tofali jingine wakajikuta wanapaniki.

Hii ilianza kutokea kule kwa Walker ambae alimpa Salah goli la ufunguzi na zaidi lile la Oxlade-Chamberlain ilikuwa ni rahisi sana kabla ya mabeki kupoteana na kuwa vipofu walio paniki na kupaniki ndio kuliendelea kufata
Lile goli la pili kwenye dakika ya 21 ilibadilisha uhalisia ya mchezo kabisa na kubadili hsia za Guardiola kabisa mda huo huo na kumfanya kuwa na mawazo, hasira ata kwa timu yake. Vitu kama hivo vinaleta ubaguzi sana na kupoteza mawasiliano ata kama wangepigana vipi, tunajuaga siku zote yupo chana na siku zote Guardiola anawatakaga wachezaji wake wasitoke nje ya game plan mpaka mchezo unaisha hii inamaanisha hakuna kurudi nyuma ni kusonga mbele tuu.
![]() |
| wachezaji wa Liverpool na kocha wao wakishangilia ushindi. |
Labda walikuwa hawajakubaliana na maamuzi ya kocha wao kwa siku ya jana kwasababu Guardiola wazi kabisa alifanya makosa kwenye kikosi chake cha kwanza kilichoanza kwa siku ya jana.
Kumbuka Klopp kabla ya mechi alinukuliwa akisema kocha mshindani mwezake kutoka Hispani ni mzuri sana kushinda ata yeye alikuwa yupo sawa kwasababu ni moja kati ya mbinu za kujitetea na kuteka akili za watu na siku zote alijua nini anachotaka.
Guardsiola alionesha heshima kubwa sana ambayo ilipitiliza aliporudiana na Klopp ambaeni kocha alievunja rekodi yake msimu huu ya kutofungwa na timu ya kingereza ule uhamuzi wa kumuweka Raheem sterling nje na kuweka kikosi cha kuzuia ndio kilicho mponza.

Eeeh City ni wazuri wewe tena sana si unaona kipindi cha pili walivokuja waliwakaba koo majogoo japo kisu kilikuwa na kutu inabidi akubali kosa kwakweli la kumuweka Sterling nje na angemuweka De Bruyne juu zaidi na sio chini angeruhusu zile huduma za kawaida zingeendelea.
Kwa Klopp 3-0 alijua kabisa bado azitoshi na bado mchezo ulikuwa mbichi mikono yake ilikuwa ikitililika jasho huku kifua cahke kikisema mengi.


No comments:
Post a Comment