Kiungo wa Kibrazili Ramires anataka kurudi Chelsea.Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 anataka kuacha kuichezea Ligi kuu ya China katika timu ya Jiangsu ambayo alijiunga nayo Januari 2016.

Lakini Ramirez alishawahi kuwasaidia The Blues kuweza kushinda kombe la klabu bingwa ulaya na Europa pamoja na Ligi kuu bila kusahau kombe la FA.
Kwasasa Ramires amefungua milango na kukubali kuwa anataka kurudi Chelsea Alisema "Chelsea? Siku zote itakuwa muhimu kwangu na kwao pia na ninataka kurudi kuwachezea tena kabla ya kumaliza soka lake.
"Ninajua milango ya Stanford Bridge siku zote itakua wazi pale nitakapo kuwa narudi na nitapenda sana kuvaa jezi yao tena.

No comments:
Post a Comment