HIVI HAWA YANGA WANAJIAMINI NIN? - BZONE

HIVI HAWA YANGA WANAJIAMINI NIN?

Share This
Mabingwa watetezi wa Ligi kuu Tanzania bara kesho Jumatatu watakuwa na kibarua cha kucheza mchezo wa Ligi huku wakitarajia kucheza mchezo wa marudiano wa klabu bingwa Afrika.



Yanga kesho ataingia dimbina akiwa nyumbani kuumana na Stand United ambao waliwalazimisha watani zao sare ya 3-3 huku watani zao wakiomba kusogezewa mchezo wao wa ligi kuu mbele ili kupata mdaa wa kupumzika na kujiandaa kukipiga dhidi ya Al Masry ya Misri huku full back wa kulia kutokea Yanga Juma Abdul akitokea na kuwapa mashabiki zao Moyo kwamba ubingwa wa ligi kuu wanabeba na kimataifa bado wataendelea kulindima.




Beki huyo amesisitiza akiwaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kesho kuipa hamasa timu yao ili iweze kuibuka na ushindi huku akisema ubingwa unawezekana.

"Kikubwa ninaomba mashabiki wa Yanga wajitokeze katika mchezo wa kesho, uwepo wao unatupa hamasa ya sisi kupambana uwanjani. Ubingwa unawezekana, hakuna kukata tamaa" alisema Abdul.

Yanga itakuwa ina kibarua dhidi ya Stand United, mechi ambayo kama Yanga itashinda itapunguza pengo la alama kuwa 3 dhidi ya Simba inayoongoza Ligi

No comments:

Post a Comment

Pages