Kevin De Bruyne akuwa kwenye orodha ya watu walioshiriki kushinda siku ya jumamosi lakini aliweza kutoa usaidizi wa magoli matatu huku Manchester City ikiibamiza Leceister magoli 5-1 kwenye dimba la Etihad.
Mbelgiji huyu ambae ni Playmaker maestro mwenye umri wa miaka 26 na akiweka usaidizi wote wa magoli matatu.
Aliweza kuwasaidia Man city kupata ushindi na kuwapeleka vijana wa Guardiola kuwa na alama 16 kileleni na kuwaacha majirani zao ambao waliopata kipigo toka kwa Newcastle.
Sergio Auguero aliweza kutembea kifua mbele kwa kuchana nyavu mara nne lakini kiukweli bila De Bruyne ndie aliewezesha.
Kwenye usaidizi wake kwenye goli la tatu lilimfanya kumpita Lionel Messi na kupanda kwenye namba 1 ambae mtoa msaidizi bora Duniani mpaka sasa tangia msimu wa 2012-2013.
Kwa mda huo Mbelgiji huyo amecheza michezo 176 kwenye mashindano ya ligi yote na kutoa usaidizi 77.
Nafasi ya pili yupo gwiji kutokea Barcelona akiwa na usaidizi 76 kutokea kwenye michezo 190 ambayo ni michezo kama 14 akiwa amempita De Bruyne.
Cesc Fabregas anakamatia nafasi ya pili akiwa na usaidizi 65 akiwa na michezo 189 ambapo akiwa sawa na Luis Suarez pamoja na Angel Di Maria.
Aliekuwa Playmaker wa Westham Dimitri Payet na assist King kutokea Arsenal Mesut Ozil wanajiumga nafasi ya sita wakiwa na usaidizi 62.
Koke wa Atletico Madrid yeye ana 57 huku nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo yeye ana 56 ila ikumbukwe mshambuliaji wa Bayern Munich Thomas Muller ana 55 ndani ya michezo 169 kwenye Wababe wa Bundesliga tangia 2012-2013.
Home
Unlabelled
KUMBE HUYU MTOTO NOMA,AWAZIDI MESUT OZIL, LIONEL NA CRISTIANO RONALDO
KUMBE HUYU MTOTO NOMA,AWAZIDI MESUT OZIL, LIONEL NA CRISTIANO RONALDO
Share This
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Bwherever is a Tanzanian Radio Personality and Blogger who initiative Bbaseonpoint blog.
No comments:
Post a Comment