Na Bwherever,
Kusema ukweli wote inabidi tuwe na majibizano kuhusiana na mchezaji mwengine wa Spurs
.
Juventus walikuwa kwenye wakati mgumu sana hasa Giorgio Chiellin alipomuweka Harry Kane kwenye hatua sawa aliokuwepo yeye akimchukulia kama Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Neymar.
Kwahiyoo nani kwenye Sayari hii anatakiwa kufananishwa na Christian Eriksen? Nina uhakika hakuna na kama wapo basi sio wengi kama tunavo zania kwenye bara la Ulaya kwasasa.
Eriksen amekuwa ni mtu mwenye mauzauza akiwa na Spurs, alikuwa ni zaidi ya mchezaji yeyote kwenye kikosi cha Tottenham ambae alimchukua na kumfanya Mauricio Pochettino na timu yake kurudi wakitokea chuma kwa vyuma viwili bila vilainisho na kuwarudisha mchezoni.
"walikuwa ni wazuri sana kushinda ata sisi!" Ayo ni maneno yalioweza kusikika kutokea kwa mashabiki wa Arsenal ambao walioweza kuona kiwango cha majirani zao kwenye michezo ya klabu bingwa Ulaya
Mpira wake alioupiga ndani ya dakika ya 72 ambao ulikuwa mpira ulio kufa uliweza kuwafanya Spurs kupata sare ilio tamu kwenye viwanja nguli Ulaya
Alijihusisha na kichwa alichopiga kane japo alikosa.
Eriksen ni mchezaji ambae yupo juu ya mchezo wowote anaocheza anaongozaga michezo na kutia molari mbali na Kevin De Bruyne anachokifanya kwa man city.
Kila mtu anakubali umuhimu wa De Bruyne ambae yupo city na wanafikilia Kane kama mchezaji muhimu kwa Tottenham.
Lakini ki ukweli kwanba Eriksen uhusiano wake na kuelewana na Kane ni muendeshaji mzuri wa Tottenham. Eriksen anauwezo mkubwa sana akiwa uwanjani Juventus ata awakumuangalia kwa umakini na hii ndio kilichofanya yeye kuweka sawa kiwango chake ambacho alikionesha kwamba yeye ni bora Ulaya.
Baada ya dakika nane tuu Spurs waliweza kupotea kwa magoli 2-0 magoli yakiwekwa kimiyani na Gonzalo Higuan lakini Eriksen aliweza kusaidia timu yake na kuyarudisha yote kwa kiwango ambacho akikiweza kuonwa na watu milioni Duniani.
No comments:
Post a Comment