'ATAKAE KUJA NI PIGA HATOKUWA BINADAMU' JOSHUA AMWAGIA MKWALA MZITO KABLA YA PAMBANO LAO CARDIFF - BZONE

'ATAKAE KUJA NI PIGA HATOKUWA BINADAMU' JOSHUA AMWAGIA MKWALA MZITO KABLA YA PAMBANO LAO CARDIFF

Share This
Bondia wa uzito wa juu nchini New Zealand, Joseph Parker ameonekana akimtafuna samaki mbichi kwa jaziba kitendo kilichotafsiriwa kuwa yupotayari kupigana na Anthony Joshua katika mpambano wao wa ubingwa wadunia wa WBA, IBF, WBO na IBO utakaofanyika Machi 31 ya mwaka huu. 

Huku Joshua akimpiga mkwala mzito mpinzani wake huyoo kwamba atakae kuja kumdondosha atakuwa sio mtu wa kawaida.

Parker mwenye umri wa miaka 26 ambaye anarekodi ya kutokupigwa hata pambano moja kati ya 24 aliyoshuka ulingoni amenuwia kuvunja rekodi ya Joshua siku hiyo. “Nimeamua kumtafuna samaki huyu mbichi maeneo ya kchwani na kumuua, bingwa wa dunia wa WBO lazima ukumbuke hili,”amesema Parker ikionekana kama mkwara kwa bondia mwenzake Anthony Joshua ambaye anatarajia kukutana nae katika ulingo mwezi Machi.

No comments:

Post a Comment

Pages