HUYU NDIO REFA ATAKAE CHEZESHA MCHEZO KATI YA SIMBA VS MBAO LEO DODOMA - BZONE

HUYU NDIO REFA ATAKAE CHEZESHA MCHEZO KATI YA SIMBA VS MBAO LEO DODOMA

Share This
SPORTS: REFA wa Dodoma, Ahmed Kikumbo ndiye atakayechezesha fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), au Azam Sports Federation Cup (ASFC) kesho Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Fainali ya ASFC itazikutanisha Mbao FC na Simba Leo Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kuanzia Saa 10.00 jioni.
Na Kikumbo atasaidiwa na Mohammed Mkono wa Tanga na Omary Juma wa Dodoma wakati mwamuzi wa akiba ni Florence Zablon pia wa Dodoma wakati Kamishna wa mchezo huo atakuwa Peter Temu wa Arusha. 

TFF inazitakia timu zote, Simba, Mbao, Waamuzi pamoja na Kamishna wao pamoja na wanafamilia wa mpira wa miguu, mchezo mzuri wenye fanaka kwa kila upande.
Bingwa wa Kombe la TFF, atajinyakulia kitita cha Sh. Milioni 50 kutoka kwa wadhamini, Azam TV na pia ataiwakilisha nchi katika Kombe la Shirikisho la Soka Afrika mwakani.

No comments:

Post a Comment

Pages