Harry Kane amekuwa ni moja ya wachezaji kwenye ligi kuu ya Uingereza wanaingiza mpunga mrefu baada ya kusaini mkataba mpya ambao utamuweka Tottenham mda mrefu kidogo huku mkataba huo ukiwa na thamani Pauni Milioni 90.
Mwaka 2016 Kane alikubali kulipwa Pauni 110,000 ambao mkataba huo wa mshahara huo ulikuwa unakimbilia mpaka 2022 lakini Spurs wanajiandaa kuhamia kwenye uwanja wao nahodha huyu wa Uingereza ambae amefunga magoli 41 msimu uliopita ametakiwa kuwa moja ya wachezaji ghali kwenye klabu yake.
Kwasasa mshahara wa Kane umeongezeka mara mbili ambapo atakuwa analipwa Pauni 200,000 kwa wiki akiwa na Bonus ambayo itakuwa inakaribia Pauni 300,000 kama mshambuliaji huyu mwenye umri wa miaka 24 ataendelea kushinda magoli.
Dili hili jipya la Kane linakuja likitokea nyuma ya kocha wake Pochettino ambae teyari ameshathibitisha maisha yake kwa Spurs kuwepo mbele kwa miaka mitano na teyari kocha huyu ameshaanza mazungumzo ya kumsawishi kiungo wake Eriksen na Ali kwenye madili yao mapya.
Home
Unlabelled
Ni Tabasamu tu ndio linasema kila kitu..!! Kane amwaga wino kwenye dili jpya Spurs mpaka 2024..
Ni Tabasamu tu ndio linasema kila kitu..!! Kane amwaga wino kwenye dili jpya Spurs mpaka 2024..
Share This
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Bwherever is a Tanzanian Radio Personality and Blogger who initiative Bbaseonpoint blog.
No comments:
Post a Comment