Bayern Munich hawakuonesha kile kiwango chao na zile swaga zao walionesha walipocheza na Borusia Dortmund ambao waliwachapa 6-0 lakini hawakutaka kufanya kwa Sevilla hasa walipokuwa ugenini waliwapa mawili tuu ya kusumbua akili zao.
Pablo sarabia ndie aliyekuwa kwanza kufungua mlango wa magoli kwa sevilla kwa kuipa Sevilla goli la uongozi . Bayern walionesha baadhi na kati ya kiwango chao kwenye mashindano haya kwa kuwaacha nje Arjen Robben pamoja na James Rodriguez. Lakini ndani walikuwa na Frank Ribery ambae ana umri wa miaka 34 lakini alicheza namba 7 kama bado kijana
Sevilla walianza kwa kujiamini kwa kuzalisha penati iliowapa goli, baada ya kipindi cha pili kuanza Sevilla walirudi tena na Moto ule ule lakini ikafikia mda bayern ikabidi wavae uhusika wa nyumbani
ambapo mnamo mwa dakika ya 68 Bayern waliweza kujipatia bao la pili kupitia Thiago Alcantara
na kufanya mchezo uweze kumalizika kwa 1-2.
No comments:
Post a Comment