Mchezaji huyo wa Taifa la Poland ambae amekuwa kwenye kiwango kizuri kwa mara nyingine tena akiwa na Bayern msimu huu anaangalia maisha yake ya soka ataenda kumalizia wapi na wakati huo huo yeye binafsi akiwa anaiota Bernabeu.
Gazeti la Uhispania limetoa taarifa ya kuwa mshambuliaji huyo ataiambia Bayern kwamba yeye a nataka kuondoka baada ya msimu huu kuisha na kuweza kutimiza ndoto zake za kutua Bermabeu,
Kama Lewandowski akiondoka Ujerumani atakuwa amewapa pigo kubwa sana Bavarians. Wakati huo mshambuliaji wao ambae ameshinda magoli 100 kwenye michezo 121 kwenye klabu yake huku miamba hiyoo ya Ujerumani watatakiwa wazibe pengo ilo kwa haraka sana kwa kuwachungulia watu kama Alvaro Morata, Edison Cavan na Timo Werner
No comments:
Post a Comment