Nyota Real Madrid alichukua tuzo hiyo mbeole ya washindani wake kutokea Fc Barcelona na Paris saint Germain nyuma ya ushindi wa kombe la La liga na klabu bingwa ulaya msimu uliopita.
Ronaldo ameshinda magoli 44 kwa klabu yake na taifa lake pia 2017 na ameshinda mara mbili kombe la klabu bingwa ulaya huku Real madrid wakivunja rekodi ya kubeba kombe ilo mara 12.
Baada ya kupokea tuzo Ronaldo alifunguka kwa kusema: "Ahsante sana wote kwa kunipigia kula " aliendelea kwa kusema "ningependa kujua uwepo wa lionel Messi na Neymar, pia kuwashukuru mashabiki wote wa Real Madrid, wachezaji wenzangu, kocha na raisi wa timu yangu napenda kusema tena ahsante."
Messi amepata magoli 50 akiwa na Barca na timu yake ya taifa Argentina ambapo Neymar ambaye ndiye mchezaji ghali kwasasa alietoka Barcelona kuelekea PSG kwa gharama ya pauni milioni 198 akiwa na magoli 25 na taifa lake.
No comments:
Post a Comment