USAJILI WA BARCELONA PAUNI 96, OUSMANE DEMBELE ATAKAA NJEE KWA MIEZI MINNE - BZONE

USAJILI WA BARCELONA PAUNI 96, OUSMANE DEMBELE ATAKAA NJEE KWA MIEZI MINNE

Share This
SPORTS: Klabu ya Barcelona leo imetangaza rasmi kuwa mchezaji wake, Ousmane Dembele atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu hadi minne kutokana na majeraha ya misuli ya paja aliyoyapata  wikiendi iliyopita kwenye mchezo dhidi ya Getafe. Kupitia tovuti ya klabu ya Barcelona imethibitisha taarifa hizo na kuandika kuwa kesho Jumanne tarehe 19 septemba, Dembele atasafirishwa kwenda Finland kufanyiwa upasuaji.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa dau la Euro milioni 160 akitokea Borussia Dortmund alitua Barcelona kama mbadala wa Neymar ambaye ameihama klabu hiyo na kujiunga na klabu ya PSG ya Ufaransa. Tazama video hapa chini jinsi Dembele alivyoumia

No comments:

Post a Comment

Pages