NA BWHEREVER
SPORTS: Wachezaji wa Asernal waendelea kujifua zaidi ili kuwakabili vijana wa west brom . Washika bunduki hao wa london wataahumana na west brom katika usiku wa Jumatatu huku wakijitahidi kujazia nyama yenye viungo vilivonona. Huku wakiwa wanatakiwa lazima washinde kwenye mchezo huo huku wakiwa wanajua wababe wa Manchester wote wakiwa kileleni mwa ligi.
Kama inavofahamika west Brom sio watu wa kuwabeza sana na kuwadharau maana huwa wanafanyaga kile wanachotumwa.
katika kujifua huko Mesut Ozil aliweza kuonekana akijiunga na washika bunduki wenzake na ikitolewa taarifa kurudi katika kikosi hicho Emirates, mjerumani huyo alikuwa akisumbuliwa na goti lakini hivi sasa amerudi katika mazoezi
, huku Theo Walcot hakionekana yupo fiti kuminyana na West Brom ukiachilia mbali na kufosiwa kutoka katika kombe la Carabao zidi ya Doncaster.Mshambuliaji Danny Welbeck, Francis Coquelin, and Santi Cazorla watakosa mchezo huo wakiwa wanasumbuliwa na majeruhi bado. Calum Chambers yeye akiwa bado anasumbuliwa na nyama za makalio na kumfanya kuendelea kukaa nje
Hiki ndio kikosi kinacho tazamiwa kucheza kesho Cech, Ospina, Mertesacker, Holding, Koscielny, Monreal, Mustafi, Bellerin, Nelson, Kolasinac, Ramsey, Wilshere, Xhaka, Elneny, Ozil, Giroud, Walcott, Sanchez, Iwobi, Lacazette.
Home
Unlabelled
ASERNAL WAENDELEA KUTENGENEZA NYAMA YENYE VIUNGO TELE! WALA TIZI LA KUFA MTU ILI KUWAKABILI WEST BROWI
ASERNAL WAENDELEA KUTENGENEZA NYAMA YENYE VIUNGO TELE! WALA TIZI LA KUFA MTU ILI KUWAKABILI WEST BROWI
Share This
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Bwherever is a Tanzanian Radio Personality and Blogger who initiative Bbaseonpoint blog.
No comments:
Post a Comment