Katika mabao hayo ya Aguero ya liyovunja mwiko kwa Watford kutofungwa katika Ligi msimu huu pia mchezaji mwingine wa City aliyefumania nyavu ni Gabriel Jesus aliongeza bao la tatu likiwa ni lake la tano msimu huu baada ya kufunga bao zuri kutokana na pasi iliopigwa na muargentina huyo.
Muargentina mwingine anayechezea nafasi ya mlinzi wa kati, Nicolas Otamendi alifunga kwa kutumia kichwa kutokana na kona iliopigwa na David Silva kabla ya Aguero kufunga bao lake la tatu, baada ya kuvamia ngome ya Watford akiwa pekee ndani ya eneo hatari.
Wakati karamu ya mabao ya City ikihitimishwa na kiungo wa timu ya taifa ya Uingereza, Raheem Shaquille Sterling aliyefunga bao la sita kupitia mkwaju wa adhabu ya penati.
No comments:
Post a Comment