ENTERTAIMENT: Ukitaja couples maarufu kwenye muziki hapa Tanzania, huwezi kuacha kuitaja ya Barakah The Prince na Naj. Wawili hao wameendelea kuwa imara kama kisiki cha mpingo, Barakah amefunguka kuhusiana na jinsi Naj alivyo msichana na tofauti na aliyefanikiwa kumbadilisha. “Naj ni yule mwanamke ambaye mimi nilikuwa namtaka,” amesema. “Unajua Naj ukimuona unaweza ukamchukulia demu fulani sister duu sana au mwanamke wa mjini kwa kumwangalia. Najma kanishangaza sana, tofauti sana na watu wanavyomfahamu. Ni fighter, ni mtu ambaye yuko in future sana yaani kila anachokifanya kwenye maisha yake ni kwaajili ya future yake,” ameongeza. “Ni mshauri wangu mkubwa sana, kaweza kunibadilisha sana mimi, kitabia kila kitu kaweza kunibadilisha. Ni vigumu sana kumwacha mtu wa hivyo tena pasipo na sababu.
”Barakah amesema hawajawahi kuachana zaidi tu ya kukosana kwa siku chache kitu ambacho anaamini hutokea kwa couples zote.
Home
Unlabelled
NAJ AMENIFANYA KUWA MWANAUME BORA -BARAKAH THE PRINCE
NAJ AMENIFANYA KUWA MWANAUME BORA -BARAKAH THE PRINCE
Share This
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Bwherever is a Tanzanian Radio Personality and Blogger who initiative Bbaseonpoint blog.
No comments:
Post a Comment