
Mchezaji huyo ambae alisajiliwa kwa ada ya pauni milioni 89 amekuwa chini ya kiwango tangia alipotoka kwenye majeruhi mwezi wa Novemba ni zaidi ya miezi miwili
Pogba ameweza kuanza michezo mitatu tuu kati ya michezo tisa tangia hausishwe kwenye dili la kuuzwa Januari na uhusiano kati ya wawili hawa kutokua vyema.

Kocha huyo amefunguka na kusema Pogba asilete visingizio vyovyote kwa kiwango chake alichokuwa nacho na asije akasingzia kuwa ni majeruhi ndio yamemfanya awe hivo.

Kocha wa Ufaransa Didier Deschamps aliweza kusema Pogba na Mourinho wiki iliopita kwa kusema ‘siwezi kuwa na furaha kuwaona wakiwa vile’

Pogba alishinda goli lake la kwanza kwenye klabu au taifa ni zaidi ya miezi minne akipiga mkwaju mkali hadi wavuni dhidi ya Russia lakini Mourinho hakuweza bado kumpamba hata kama alishinda goli ilo...
Pogba atakua anajipa matumaini kuweza kuanza leo kwenye kikosi ambacho kitaweza kucheza na Swansea kwenye dimba la Old Trafford na Luke shaw anaweza akawepo kwenye kikosi pia baada ya Ashley Young kupata majeraha ya goti kwenye kampeni ya Uingereza
No comments:
Post a Comment