Mshamnuliaji wa washika mitutu bado hajaweza kupata nafasi ya kuanza kwenye kikosi chake kwenyebmichezo ya ligi kuu msimu huu kwa michezo yake mingi anayokywa anaanza ni kwenye ligi ya Europa.
Lakini mfaransa huyo ameweza kuleta taswira na matokeo yaliyo bora kwa timu yake siku ya Jumapili akitokea benchi na kuweka mpira wavuni ndani ya dakika ya 88 na kusawazishabdhidi ya Southampton.
Giroud alikuwa anakaribia kuhama klabu baada ya usajili wa Alexandre Lacazette lakini akaamua kubaki na kupigania nafasi yake.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 goli lake dhidi ya saints limeweka rekodi mpya ya mchezaji mwenye magoli mengi akitokea benchi kwa timu moja.
Akiongea na Arsenal.com, Wilshere alisema ‘Inaonesha ukubwa na upana wa kikosi chetu. Kwa mimi Oli ni moja kati ya washambuliaji wazuri kwenye ligi kuu akiwa ndani na akiwa nje kwenye benchi kwahiyo inaonesha nini tulicho nacho kwasasa.’
‘Kuna michezo mingi sana mwezi huu wa Disemba nina uhakika utaenda kuanza kama anaingia akitokea benchi na kushinda magoli iyo inafurahisha sana hasa kwa timu na lilikuwa goli muhimu kwake yeye’
No comments:
Post a Comment