“Kiukweli nina Furaha sana kujiunga na Arsenal, Arsenal ni Klabu kubwa na ni kongwe sana. Sababu ya kujiunga na Arsenal ni kutokana na Mafanikio ambayo wachezaji wa Ufaransa wamekua wakipata hapa, kama vile Thierry Henry pamoja na wachezaji wengine kutoka Ufaransa lakini pia kocha yupo katika klabu hii kwa muda mrefu na kuna wachezaji baadhi kutoka Ufaransa ambao bado wanafanya vizuri pia na nipo tayari kuisaidia Arsenal ili ishinde mataji mengine”. Alisema Lacazette.
Nyota kadhaa kutoka Ufarana wamewai kuitumukia Arsenal kwa Mafanikio makubwa wakiwemo Patric Viera William Gallas, Robert Pires pamoja na Thierry Henry ambao miongoni mwao walikuwepo katika kikosi cha Arsenal kilichotwaa ubingwa bila kufungwa msimu wa 2003-2004.
No comments:
Post a Comment