WARRIORS WAZIKUENDELEZA UBABE DHIDI YA CAVS....... - BZONE

WARRIORS WAZIKUENDELEZA UBABE DHIDI YA CAVS.......

Share This
SPORTS: Timu ya mpira wa kikapu ya Golden State Warriors kutoka ukanda wa Magharibi wameendeleza ubabe mbele ya Cleveland Cavaliers kutoka Mashariki baada ya kuibuka na ushindi katika mfululizo wa fainali za NBA ikiwa ni mchezo wa pili uliopigwa katika dimba la Oracle Arena.
Photo published for Game 2 Preview: Warriors vs. Cavaliers - 6/4/17 | Golden State Warriors
Warriors wameibuka na ushindi wa vikapu 132-113 dhidi ya Cavs ukiwa ni mchezo wa 14 mfululizo kwa Warriors bila kupoteza pia ni ushindi wa pili kwa Warriors katika fainali hizi za mwaka 2017 dhidi ya Cavs.
Katika mchezo huo uliopigwa usiku wa kuamkia leo rekodi kadhaa zimevunjwa na nyingine kuwekwa ikiwemo ya LeBron James wa Cavaries kuwa mchezaji wa pili katika historia ya wachezaji wenye pasi nyingi za mwisho “assist” katika historia ya fainali za NBA huku Stephen curry na  Kevin Durant wa Warriors wakiweka rekodi ya kuwa wachezaji wa kwanza kutoka timu moja kufikisha usawa wa alama zaidi ya 30 katika mechi mbili za mwanzo za fainali za NBA.
Ushindi wa Wariors usiku wa jana ulikua ni furaha kwa kocha wao Steve Kerr ambae alirejea katika timu kwa mara ya kwanza tangu Aprili 19 kutokana na kusumbuliwa na maradhi.

No comments:

Post a Comment

Pages