


Beki huyo,25 amekuwa akihusishwa kuhamia Liverpool tangu msimu uliopita kwa ada ya uhamisho inayokadiriwa kuwa ni Paundi milioni 50 licha ya kuwa na mkataba na Southampton wa miaka 6.
Muholanzi huyo hajaonekana uwanjani kipindi cha miezi mitano tangu alipopata majeraha katika mchezo waliopoteza kwa magoli 3 dhidi ya Leicester City Januari 22, amekosa michezo mingi ukiwemo wa fainali ya EFL Cup dhidi ya Manchester United Mwezi Februali mwaka huu.
Southampton pia imeripoti kuwa itagomea ofa yoyote maalumu itakayoletwa na Liverpool ikigundua ilianza mazungumzo na mchezaji huyo kabla.
No comments:
Post a Comment