DEONTAY WILDER KUSHATIKIWA KWA TUHUMA ZA BANGI - BZONE

DEONTAY WILDER KUSHATIKIWA KWA TUHUMA ZA BANGI

Share This
SPORTS: Bingwa wa ndondi za uzani mzito duniani anayeshikilia taji la WBC Deontay Wilder ameshtakiwa kwa kumiliki bangi. Maafisa wa polisi katika eneo la Tuscaloosa jimbo la Alabama wamesema kuwa alikamatwa alipokuwa akiendesha gari lenye vioo linalomficha aliye ndani yake kuoinekana.
Maafisa wanasema kuwa walipata dawa hiyo ndani ya gari lake.
Wakili wa Wilder Paul Patterson aliambia kitengo cha habari cha Tuscaloosa kwamba dawa iliopatikana ndani ya gari hilo haikuwa yake na kwamba mtu mwengine alitumia gari hilo wakati bondia huyo alipokuwa safarini.
Aliambia chombo hicho kwamba Deontay amekuwa safarini kwa siku kadhaa.
Wilder alishtakiwa na polisi na kuachiliwa huru kwa dhamana ya dola 1000.
Maafisa walipata ruhusa ya kulisaka gari hilo kabla ya kufanikiwa kupata kiwango cha bangi kutoka kwa gari hilo, taarifa ya maafisa wa polisi wa Tuscaloosa ilisema.
Pigano la mwisho la Wilder lilikuwa la ushindi wa raundi ya tano kwa njia ya Knockout dhidi ya Gerlad Washington alipotetea taji lake la WBC ambalo amemiliki tangu 2015.

No comments:

Post a Comment

Pages